Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Umewaangusha Wakenya, Millicent Omanga amwambia Uhuru

Bd77fea09c0aa942 Umewaangusha Wakenya, Millicent Omanga amwambia Uhuru

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Milicent Omanga alisema utawala wa sasa unaelekea pabaya kwa sababu ya ufisadi mkubwa ambao umekumba serikaliOmanga alibaini kuwa Rais Uhuru Kenyatta aliwahi kukiri kwamba serikali yake ilikuwa imeoza na ufisadi, lakini hakutoa suluhishoHaya yanajiri miezi michachee tu baada ya kiongozi wa taifa kukiri kwamba KSh 2 bilioni zinaibwa katika serikali yake kila kuchaoSeneta Mteule Millicent Omanga amesema kwamba serikali ya Rais Uhuru Kenyatta imewaangusha Wakenya kwa njia nyingi akidai kwamba imejaa ufisadi.

Omanga alisema utawala wa Uhuru umetikiswa na ufisadi mkubwa na kwamba nchi inaelekea pabaya.

Mbunge huyo alisema kwamba kiongozi wa nchi wakati mmoja alikiri kwamba serikali yake ilikuwa imeoza na ufisadi mkubwa lakini hakutoa suluhisho.

"Kuliongozi wa taifa amekiri kwamba serikali yake imeshamiri ufisadi lakini hana sukuhisho kuhusiana na ndonda ndugu hilo. Hatuwezi shukishwa kwa kiasi hicho. Tunapaswa kuchukua usukuani wa kuendesha nchi yetu sisi wenyewe. Labda kabla ya 2022 kwa sababu tunaipoteza," jumbe wake Twitter ulisema.

Haya yanajiri wakati Wakenya wengin wanalia sababu ya ufisadi unaoendeshwa na walioshikilia nyadhifa kuu serikalini ambao wanairudisha nchi nyuma.

Mapema mwaka huu, TUKO.co.ke iliripoti kwamba rais aliwaacha Wakenya wakiwa machungu vinywani mwao baada ya kusema waziwazi kwamba KSh 2 bilioni zinaibiwa kila siku katika serikali yake.

Rais, ambaye mara kwa mara amesisitiza kujitolea kwake kupigana na ufisadi katika serikali ya Jubilee, alikiri kwamba nchi ilikuwa ikipoteza zaidi ya KSh 2 bilioni kila siku kwa ufisadi.

Wakati huo kiongozi wa taifa alitetea mchakato wa maridhiano wa (BBI) ambao unahitaji bajeti kubwa kuufanikisha.

"Bado hatujui ni kiasi gani kura ya maoni ya BBI itagharimu kwa sababu bado hatujafikia hatua hiyo. Pesa wanazoiba kila siku ni zaidi ya KSh 2 bilioni ya kura hiyo ya maoni."

Watu hawa (wanaopinga BBI) hawana dhihaka. Wacha tuzingatie kile kitakachokukinga wewe na watoto wako. Sikulazimishi kuwa na mimi lakini usiamini mtu yeyote ana njia njema, "alisema.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke