Jumba la Jiji la Nairobi - mji mkuu wa Kenya - limekuwa jengo la kwanza la serikali barani Afrika kuthibitishwa kama jengo la kijani na Shirika la Fedha la Kimataifa la Word Bank (IFC).
"Hatua muhimu katika maendeleo ya jiji la Nairobi," IFC Africa ilisema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Green Building Society la Kenya Nasra Nanda alisema Nairobi imeweka kiwango kipya cha maendeleo ya miji, akisisitiza umuhimu wa mazoea endelevu katika kuunda miji ya siku zijazo.
Katika sherehe ya kuadhimisha hafla hiyo, gavana wa kaunti ya Nairobi Sakaja Johnson alitoa shukrani kwa kila mtu aliyewezesha Jumba la Jiji kufikia hatua hiyo muhimu.