Tue, 24 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kwa mujibu wa Sheria mpya zilizopitishwa katika Jiji la Nairobi nchini Kenya, iwapo utakutwa unatema mate au kupenga mafua jijini humo basi utalazimika kulipa fedha ya Kenya KSh 10,000 sawa na Sh 200,000 za Kitanzania.
Sheria hiyo imekuja baada ya kaimu gavana wa Jijini humo, Anne Kananu, kusaini sheria itakayo dhibiti vitendo hivyo katika maeneo ya Umma.
Adhabu nyingine kwa watakao kiuka sheria hiyo ni kifungo cha miezi sita jela, adhabu hizi zote ni kwa wenyeji na wageni wa jijini humo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live