Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uhuru awaonya Wakenya dhidi ya kuwachagua wezi

Ce7d38effead5c00 Uhuru awaonya Wakenya dhidi ya kuwachagua wezi

Sat, 30 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta amewaonya Wakenya dhidi ya viongozi aliowataja kuwa wezi na walaghai, ambao amesema taifa haliwezi kuwa salama mikoni mwao. Uhuru alitoa wito kwa Wakenya kumchagua kiongozi anayeaminika ambaye atakuwa na nia ya kuendeleza urithi wake baada ya kumalizika kwa muhula wake wa pili na wa mwisho.

Rais Kenyatta bado hajamtaja mrithi anayempendelea licha ya uhusiano wa karibu na Raila Odinga wa ODM ambaye pia bado hajatangaza rasmi kuwania urais 2022.

Kulingana na Uhuru, taifa linastahili kiongozi ambaye hataangusha urithi wake au kuhatarisha msingi wa kiuchumi uliojengwa awali na rais mstaafu Mwai Kibaki.

Rais alikuwa akihutubia wakazi wa mji wa Ruiru mnamo Ijumaa, Oktoba 29, baada ya kuhudhuria hafla ya gwaride katika eneo hilo.

Akizungumza kwa lugha yake ya mama, Uhuru aliwataka Wakenya kuwa makini na wanasiasa wanaojitokeza kuwachochea badala ya kuuza manifesto zao ambazo zitabadilisha nchi na kuendeleza kazi zake.

"Msikubali kuchochewa na wanasiasa. Tafuteni na mchague viongozi wanaothamini amani, watakaoleta Wakenya pamoja, watakaohakikisha mwendelezo wa miradi ya maendeleo tuliyoanzisha," rais alisema.

Rais alipendekeza kuwa mtangulizi wake alianzisha msingi dhabiti wa kiuchumi ambao utahitaji kiongozi anayeaminika ambaye atajenga hata zaidi.

Uhuru amekuwa akisisitiza kwamba kamwe hawezi kuliwacha taifa mikononi mwa wale ambao anahisi ni wezi.

"Tusirudi tena tulikotoka. Nawasihi, msiruhusu miaka 10 ya Mzee Kibaki na miaka yangu 10 kutumbukia shimoni kwa kuwachagua wezi na mafisadi," Uhuru alisema.

Hata hivyo, rais hakumtaja haswa mrithi wake anayependelea licha ya wapambe wake kuonyesha waziwazi kwamba anamlenga aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga.

Wakati wa hotuba yake huko Ruiru, alipongeza mapatano ya Machi 2018 aliyoafikiana na Raila akisema nchi inahitaji amani.

Wakati uo huo, Uhuru alionekana kumtetea kiongozi huyo wa ODM ambaye baadhi ya wanasiasa wa Mlima Kenya na ambao ni washirika wa Naibu Rais William Ruto wamekuwa wakimwamini

"Msipotoshwe au kuchochewa kuhusu kiongozi huyu au yule. Taifa hili ni letu sote. Ikiwa kuna matatizo au vurugu, ni sisi huwa wahasiriwa. Tusikubali kamwe kurudi nyuma," rais alisema.

Wiki mbili zilizopita, Uhuru alimkashifu kwa njia isiyo ya moja kwa moja naibu wake ambaye alikuwa amemtaja kama "tapeli".

Akizungumza na umati wa watu mjini Sagana mnamo Jumatatu, Oktoba 18, rais aliwataka wenyeji kumsikiliza kila mgombea urais anayetembelea eneo hilo kwa umakini na kukagua sera zake.

"Nyie watu mnadanganywa sana, kwanini msiwaambie mnachotaka ni maendeleo? Watu wangu amkeni mjue mambo yatakayowasaidia nyinyi na vizazi vyenu," alisema huku akishangiliwa na wananchi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke