Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uhuru amemteua Monica Juma kuwania Ukatibu Mkuu Jumuiya ya Madola

1dfd6de8a7854718 Uhuru ampendekeza Monica Juma kuwania kiti cha katibu mkuu Jumuiya ya Madola

Tue, 31 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta amemteua Waziri wa Ulinzi, Monica Juma kuwania kiti cha katibu mkuu wa Jumuiya ya Madola.

Awali, Juma alihudumu kama katibu mkuu katika wizara za Ulinzi na Masuala ya Kigeni.

Rais Uhuru Kenyatta alisema Monica Juma ana rekodi nzuri ya utendakazi akionyesha matumaini kuwa atashinda kiti hichoIwapo atashinda kiti hicho, Juma atalazimika kujiuzulu kama waziri ili kuongoza shirika lenye wanachama 54 wakoloni wa Uingereza.

Iwapo atashinda kiti hicho, Juma atalazimika kujiuzulu kama waziri ili kuongoza shirika lenye wanachama 54 wakoloni wa Uingereza lenye makao yake jijini London.

Katika taarifa siku ya Jumatatu, Agosti 30, Rais Kenyatta alisema Monica Juma ana rekodi nzuri ya utendakazi akionyesha matumaini kuwa atashinda kiti hicho.

“Sina shauku kuwa Monica Juma atakuwa mgombeaji bora. Juma ana rekodi nzuri ya uongozi, ubalozi na uzoefu wa serikali za kanda na kimataifa, maendeleo ya kimataifa, usalama na masuala ya kibinadamu," ilisoma sehemu ya taarifa hiyo.



Read also

Magazeti Jumanne, Agosti 31: Uhuru Kuwapiga Kalamu Baadhi ya Marafiki Zake Mawaziri

Uhuru pia alimsifu Juma kama mwanadiplomasia bora akiongeza kuwa alifanya kazi nzuri katika idara zote alizosimamia.

“Ni matumaini yangu kuwa Marais wa Mataifa ya Dola (CHOGM) watapendelea uteuzi huu," aliongezea.

Awali, Juma alihudumu kama Katibu Mkuu katika wizara za Ulinzi na Masuala ya Kigeni.

Kisha baadaye alipandishwa ngazi kuwa Waziri wa Masuala ya Kigeni kabla ya Kuhamishwa hadi Wizara ya Ulinzi ambapo anahudumu sasa.

Manoah Esipisu ateuliwa mwenyekiti wa Jumuiya ya MadolaKatika taarifa nyingine, Balozi wa Kenya nchini Uingereza Manoah Esipisu aliteuliwa kuongoza Kamati Maalum ya Bodi ya Magavana wa Jumuiya ya Madola.

Wizara ya Masuala ya Kigeni ilithibitisha kuwa Esipisu alichaguliwa na wanachama 53 wa Jumuiya ya Madola.

Esipisu alimrithi mwenzake Ellison Greenslade, ambaye ni Balozi wa Bahamas nchini Uingereza.

Kabla ya kuteuliwa balozi, Esipisu alihudumu kama msemaji wa Ikulu nchini hadi Machi 2019 wakati alipata wadhifa mpya.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Mwanafunzi Mkenya Mwenye Umri wa Miaka 98, Atua Ufaransa Kuhudhuria Mkutano wa Rais Macron

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke