Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uhuru aingia katika kituo cha radio usiku bila kutarajiwa na kusalimu mashabiki

2d32b2c475ff097c Uhuru aingia katika kituo cha radio usiku bila kutarajiwa na kusalimu mashabiki

Wed, 7 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta alikuwa ameandamna na mkuu wa NMS Mohamed Badi kuzuru mitaa kadhaa usiku jijini Nairobi Wakati wa ziara hiyo, Rais alifungua hospitali tano katika vitongoji duni na kushuhudia namna vituo hivyo vya afya vitakuwa vikitoa huduma usikuBaadaye usiku huo, aliingia katika kituo kimoja cha radio mtaani wa Mukurwe kwa Reuben na kuwasalimu wasikilizaji

Rais Uhuru Kenyatta ametembelea mitaa kadhaa katika kaunti ya Nairobi kukagua miradi ya serikali.

Kiongozi huyo wa taifa usiku wa Jumanne, Julai 6, alijitokeza akiwa amevalia jaketi ya kijeshi akiandamana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Huduma la Jiji la Nairobi (NMS) Mohammed Badi na viongozi wengine.

Katika picha zilizopakiwa mtandaoni, Rais alifungua hospitali kadhaa ikiwemo Hospitali ya Gichagi-Kangemi, Zahanati ya Gatina na zingine tatu katika vitongoji duni vya Nairobi.

“Zahanati hizo na hospitali zitatoa huduma saa 24 ili kupunguza msongamano katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta na Mama Lucy. Badala ya mtu kutumia nauli kuenda kutafuta matibabu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, wanatakiwa kutafuta huduma katika vituo hivyo karibu nao,” Uhuru alisema.

Ripoti zinadai kuwa hospitali hizo zitahudumu kwa saa 24, kiongozi wa taifa akishuhudia namna vituo hivyo vya afya vitakuwa vikitoa huduma usiku.

Hospitali hizo tano ni miongoni mwa vituo 24 vya matibabu ambavyo vinajengwa na NMS katika vitongoji duni jijini Nairobi.

Baadaye usiku huo, Uhuru aliingia katika kituo kimoja cha radio mtaani wa Mukurwe kwa Reuben bila kutarajiwa na kuwasalimu wasikilizaji.

Itakumbukwa kwamba hii si mara ya kwanza rais kufanya ziara yake usiku, huenda kuzuia kuvutia umati mkubwa kutokana na COVID-19.

Mnamo Juni 2020, Video ya Rais Uhuru Kenyatta na 'nduguye' Raila odinga wakikagua miradi ya barabara usiku ilisambaa mtandaoni.

Kanda hiyo ilinaswa na camera za CCTV jijini Nairobi na inaarifiwa ilikuwa ni usiku wa Juni 1 baada ya sherehe za Madaraka.

Huku wakiwa na magari mawili pekee, wawili hao walionyeshwa wakiingia jijini Nairobi usiku na kuanza kukagua miradi ya kurembesha jiji inayoendelea.

Kwenye kanda hiyo iliyopepea mtandaoni, Rais Uhuru anaonekana akishuka kwenye gari ndogo na kisha Raila kumfuata.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke