Tue, 21 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali ya nchini Uganda imepokea Chanjo milioni 1.6 mpya ya Pfizer kutoka kwa Marekani ikiwa ni hatua ya kupambana na janga la UVIKO -19
Hatua hii inatajwa kuwa kubwa tangu zoezi la ugawaji wa chanjo kuanzza nchini humo, huku idadi kubwa ya watu ikitarajiwa kuongezeka katika takwimu za waliopokea chanjo hiyo.
Hata hivyo Uganda imeshapokea Chanjo zaidi ya milioni 2.7 ambazo zinajumuisha chanjo ya Astrazeneca, Sinovac na Moderna.
Dozi hiyo mpya imewasili nchini humo kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe, kwa ushirikiano wa Umoja wa Mataifa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live