Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uganda: Madaktari wafanikiwa kumtenganisha pacha hai na mwenzake aliyeaga dunia

Af5823a43476d7f1 Uganda: Madaktari wafanikiwa kumtenganisha pacha hai na mwenzake aliyeaga dunia

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Upasuaji huo tata ulifanywa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Soroti Ijumaa, Machi 26

- Watoto hao wawili walikuwa wameungana sehemu ya tumbo

- Mama yao, Loyce Alinga, mwanafunzi wa kidato cha tatu nchini humo, alikuwa akiendelea kupata nafuu katika kituo hicho

Madaktari nchini Uganda wamefanikiwa kutenganisha pacha walioungana na ambao mmoja wao alikuwa ameaga dunia.

Upasuaji huo tata ulifanywa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Soroti Ijumaa, Machi 26.

Kulingana na gazeti la Daily Monitor, mama ya pacha hao alikuwa amejifungua siku iliyotangulia ya (Alhamisi) kupitia sehemu ya upasuaji, lakini mmoja wao hakuwa hai.

Watoto hao wawili walikuwa wameungana sehemu ya tumbo.

Mama yao, Loyce Alinga, mwanafunzi wa kidato cha tatu nchini humo, alikuwa akiendelea kupata nafuu katika kituo hicho.

Paulo Oluo, babu ya watoto hao, alisema madaktari walidhani watoto wote wangefariki dunia papo hapo, lakini kwa mshtuko, mmoja alikuwa hai siku sita zilizokuwa zimepita huku na walikuwa bado wamemeungana.

Katika ripoti tofauti, sherehe zilitanda katika katika Hospitali Maalum ya Wanawake na Watoto Wachanga ya Mulago baada ya madaktari kutenganisha pacha waliokuwa wameungana.

Picha 9 za kuthibitisha Upendo wa Marehemu Pombe kwa Wasanii wa Bongo

Timu ya madaktari waliobobea walitumia tu saa 20 kufanikisha upasuaji uliomalizika asubuhi ya Jumanne, Novemba 17.

Waziri wa Afya Jane Ruth Aceng na Katibu wake wa Kudumu Diana Atwine walithibitisha mafanikio hayo kupitia Twitter.

"Shukrani kubwa kwa timu yetu ya wataalamu ambao walifanya upasuaji wa masaa 20 kuwatenganisha mapacha wa Siamese katika Hospitali Maalum ya Kitaifa ya Mulago. Kujitolea, bidii na juhudi zilizowekwa na timu yetu ni bora zaidi," Aceng alisema.

Watoto hao wawili walikuwa wameungana sehemu ya makalio.

Mnamo mwaka wa 2016, timu ya madaktari waliochukuliwa kutoka Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH) na Shule ya Sayansi ya Afya katika Chuo Kikuu cha Nairobi ilitenganisha pacha walioungana waliokuwa na umri wa miaka 2.

Upasuaji huo ulichukua saa 23.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke