Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uganda: Maafisa 160 wa serikali, wabunge 14 wakutwa na maambukizi ya COVID-19

59015b89fad2e6f7 Uganda: Maafisa 160 wa serikali, wabunge 14 wakutwa na maambukizi ya COVID-19

Thu, 24 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Serikali ya Uganda imetupilia mbali madai kwamba wabunge 200 wamepatikana na virusi vya covid-19 baada ya kupimwaKulingana na taarifa kutoka bungeni, wabunge walifanya vikao vitatu na vyote, walizingatia masharti ya kudhibiti maambukizi ya virusi hivyoKufungwa kwa bunge kwa siku 14 ilikuwa moja wapo wa njia ya kudhibiti msambao wa virusi hivyoSerikali ya Uganda imefutilia mbali madai kwamba zaidi ya wabunge 200 walipatikana na virusi vya COVID-19 baada ya kupimwa.

Kupitia kwenye taarifa yake, Jumatano Juni 23, ni maafisa 160 wa serikali 14 wakiwemo wabunge ndio waliopatikana na maambikizi ya virusi hivyo.

Aidha, bunge lilisisitiza kwamba lilifanya vikao vitatu hivi majuzi na wabunge walizingatia masharti yote ya kuzuia msambao na maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo.

Haya yanajiri saa chache baada ya vyombo vya habari kutangaza kwamba zaidi ya wabunge 200 walikuwa na maambukizi ya virusi hivyo.

Kila mbunge alitakiwa kupimwa dhidi ya virusi hivyo kabla ya kuruhusiwa kuingia katika majengo ya bunge.

" Kati ya sampo zilizopimwa kwa mara ya kwanza, watu 40 walipatikana na virusi hivyo kwenye kikao cha kwanza, watu wengine 50 walipatikana na virusi hivyo kwenye kikao cha pili na wengine 70 kwenye kikao cha tatu walipatikana na virusi hivyo. Ni wabunge 14 pekee ndio waliopatikana na virusi hivyo kati ya wale waliopimwa na wala sio 200 kama ilivyoripotiwa awali.

Wabunge hao walisema kufungwa kwa bunge kwa wiki mbili ni mojawa wa njia ya kuzuia na kudhibiti msambao wa virusi hivyo.

Wakati huo huo, wabunge waliwahimiza wananchi waendelee kuzingatia masharti yaliotangazwa na Rais Yoweri Museveni.

Akihutubia taifa Ijumaa, Juni 19, Rais Museveni atangaza kufungwa kwa nchi kwa siku 42 baada ya watu 42 kufariki dunia na maambukizi 1,000 kuripotiwa kwa muda wa saa 24.

Museveni pia alipiga marufuku usafari wa magari ya umma pamoja na ya binafsi kutoka wilaya moja hadi nyingine.

Shule pia zilifungwa kwa siku 42.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke