Thu, 28 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muungano wa Afrika umeisimamisha Sudan kushiriki katika shuguli zake zote hadi mamlaka ya mpito inayoongozwa kiraia itakaporejeshwa.
Muungano huo umesema kuwa mapinduzi ya Jumatatu hayakuwa ya kikatiba. Maandamano ya kupinga kuchukuliwa mamlaka kwa jeshi yanaendelea katika siku ya tatu mfululizo katika mji mkuu Khartoum.
Abdalla Hamdok alikamatwa wakati wa mapinduzi na kufungwa kifungo cha nyumbani. Bw Blinken kwa mara nyingene tena amewataka wanajeshi walionyakua madaraka kuwaachilia huru viongozi wa kiraia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live