Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

UN waonya juu ya ongezeko la ukiukaji wa haki za binadamu DRC

Jeshi La DRC Lavishutumu Vikosi Vya Ulinzi Vya Rwanda UN waonya juu ya ongezeko la ukiukaji wa haki za binadamu DRC

Tue, 7 Nov 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kesi 940 za ukiukwaji wa haki za binadamu na dhulma mbalimbali zimerekodiwa nchini DRC kwa miezi ya Julai na Agosti 2023 pekee, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya hivi punde kutoka ofisi za pamoja za haki za binadamu za Umoja wa Mataifa (UNJHRO). Idadi inayoongezeka ikilinganishwa na miezi iliyopita, pia kunaripotiwa ongezeko kubwa la unyanyasaji wa kijinsia.

Hili ndilo jambo lililoangaziwa katika ripoti hii, ongezeko hili la waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia: Kesi 120 zilirekodiwa na UNJHRO, 49 mwezi Julai, 71 mwezi Agosti, nyingi zikiwa ni za wapiganaji wa makundi yenye silaha. Unyanyasaji wa kijinsia unaohusishwa na migogoro iliyotambuliwa kupitia tume kadhaa za uchunguzi kuhusiana na tatizo hili, unaeleza Umoja wa Mataifa, katika maeneo ambayo ni vigumu kufikiwa, kwa mfano katika majimbo ya Maniema na Tanganyika.

Na kile ambacho ni halali kwa unyanyasaji wa kijinsia pia ni halali kwa ukiukaji wa haki za binadamu na dhulma, ambao wengi wao wanawajibika kwa makundi yenye silaha. Lakini ripoti hiyo bado inabainisha kuwa mwezi Agosti, kulikuwa na ongezeko la idadi ya ukiukaji unaohusishwa na maafisa wa serikali katika majimbo ya Kivu Kaskazini, Haut-Katanga na Kinshasa. Wakati huu inahusu hasa kukamatwa na kufungwa kiholela.

Hatimaye, Ofisi ya Pamoja pia inataja ongezeko la ukiukaji unaohusishwa na uwajibikaji wa kidemokrasia. Ishara ya kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Desemba 20.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live