Sun, 17 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Uganda, Simon Byabakama amesema katika matokeo ya awali ya Uchaguzi Mkuu idadi ya kura za mgombea wa Upinzani Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’ zimefikia 34.62% huku Yoweri Museveni akiendelea kuongoza kwa 58.83%
Matokeo hayo yanaonyesha ‘Bobi Wine amepanda kwa asilima kadhaa tofauti na 27.9% ya matokeo ya jana.
Taarifa zinasema kuwa japo Museveni bado anaongoza kwa wingi wa kura, idadi kwa asilimia imepungua kutoka 61.98% iliyotangazwa na tume hiyo, matokeo ya awali kutoka vituo vya kupigia kura 30,098 kati ya 34,684 yameshatangazwa hadi sasa.
Chanzo: habarileo.co.tz