Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Twitter yachemka baada ya Makau kusema hakuna wa kukabiliana na Ruto 2022

C00eb139049b0b1c Twitter yachemka baada ya Makau kusema hakuna wa kukabiliana na Ruto 2022

Sun, 4 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Twitter iliwaka moto baada ya makala ya Jumapili ambapo Makau Mutua alisema 2022 DP atakuwa IkuluBaadhi walisema makala hayo ni ishara ya mchanganuzi huyo kutafuta namna ya kuingia KarenWanatwitter wengine hata hivyo walionya kuwa kutangulia baa si kulewa na mambo ya 2022 badoMtandao wa Twitter umewaka moto baada ya makala yaliyoandikwa na mchanganuzi Makau Mutua kumhusu Naibu Rais William Ruto.

Akiandika kwenye gazeti la Nation Jumapili Julai 4, Makau alisema amemchambua DP Ruto na kufikia uamuzi kuwa sasa hakuna anayeweza kumzuia kuingia Ikulu.

Alisema kinachosaidia kampeni ya Ruto kuingia Ikulu ni wapinzani wake kuwa watu bwege ambao wanajikokota na hawana mbinu mufti ya kukabiliana naye.

Uchanganuzi wangu unaniambia kuwa kuna nafasi kubwa kwa DP William Ruto, jamaa ambaye aliponea makali ya mahakama ya ICC kwa tundu la sindano, huenda akawa rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya," aliandika Makau kwenye makala hayo.

Ruto anaendelea kuvuma wakati ambapo wapinzani wake wanaendelea kujikokota. Wamekuwa ndio watermelons. Ndio maanaka ninatabiri kuwa ifikapo siku ya uchaguzi 2022, Ruto ataingia Ikulu asubuhi na mapema," aliendelea kuandika.

Uchanganuzi huo umewasha moto kwenye mtandao wa Twitter wengi wakisema Profesa huyo wa siasa ameanza kumpigia debe DP.

Hatua yake ilionekana kama safari ya kuingia mrengo wa DP wa Tangatanga ambapo amekuwa akikusanya 'brains' za kumsaidia kushinda uchaguzi ujao.

Baadhi hata hivyo walisema makala ya Makau ni kinaya na kuonya wandani wa DP dhidi ya kufikiria kuwa makala hayo yalikuwa kuhusu hali ilivyo.

James Olekada naye alisema huenda Makau amegeuka bloga wa Karen aliyeletwa mezani na wakili tajika Ahmednasir Abdullahi.

George Kim naye alimkumbusha kuhusu injili yake ya awali kuwa Ruto hawezi kushinda uchaguzi wa urais nchini.

Amolo G naye aliwakumbusha wote kuwa kutangulia baa si kulewa akisema siku ya kura ingali mbali zaidi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke