Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tutahakikisha Raila ni Rais hata hata bila BBI

7ce660eecb4ad3a1 Tutahakikisha Raila ni Rais hata hata bila BBI

Thu, 5 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Murathe alisema Raila Odinga haitaji kufanikiwa kwa mpango wa BBI kumrithi Rais UhuruMakamu mwenyekiti wa Chama cha Jubilee aliwaambia vijana wa Murang'a wajiandae kwa serikali itakayoongozwa na Raila OdingaRafiki wa karibu wa Raila na Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa Junet Mohammed alithibitisha kwamba Jubilee na ODM zinafanya mazungumzo ya kuunganaMakamu mwenyekiti wa Chama cha Jubilee David Murathe ametabiri ushindi mkubwa kwa kiongozi wa ODM Raila Odinga katika uchaguzi wa urais wa 2022.

Murathe, ambaye alikutana na baadhi ya vijana huko Murang'a Jumatano, Agosti 4, aliwataka wajiandae kwa serikali itakayoongozwa na Raila.

Mwanasiasa huyo alisema kiongozi wa chama cha ODM hahitaji mchakato wa maridhiano (BBI) kumrithi Rais Uhuru Kenyatta na kwamba atawashinda wapinzani wake kwa urahisi.

"Nimesema na ninarudia tena jiandaeni kwa urais wa Raila mnamo 2022. Tunapozungumza tunataka kuhakikisha Jakom ni rais na BBI iwepo au hata isiwepo," Murathe alisema.



Read also

"Ruto Atatufinya Sana": David Murathe Asema Hatakubali DP Kuingia Ikulu

Kwingineko ni kwamba Uhuru na Raila walisafiri nyakati tofauti hadi mjini Mombasa ambapo watafanya kikao cha faraghani.

Inaaminika kwamba suala la muungano wa Jubilee na ODM na vile vile siasa za urithi 2022 litaangaziwa litakuwa agenda kuu ya mkutano huo.

Murathe alisema kwamba mkutano wa Mombasa utajadili kuhusiana na suala la uchaguzi mkuu wa 2022 ambapo Raila atakuwa akichukua usukani wakati kura itakapopigwa.

Akizungumza KTN News mnamo Jumatano, Agosti 4, rafiki wa karibu wa Raila na Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa Junet Mohammed alithibitisha kwamba Jubilee na ODM zinafanya mazungumzo ya kuungana

Hata hivyo, alikuwa mwepesi kuongeza kuwa chama cha Chungwa kiko tayari kuungana na chama kingine chochote mradi tu siasa za Kenya zitaboreshwa.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

William Ruto Akiri Alifanya Kazi Kikamilifu kwa Miaka Mitano ya Kwanza Madarakani
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke