Thu, 2 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali nchini Tunisia, imeidhinisha hati ya kukamatwa kwa aliyekuwa Mgombea Urais wa Taifa hilo 2019, Nabil Karoui na Kaka yake kwa kosa la kuvuka mpaka wa Nchi kwa njia haramu. Wawili hao wamekuwa kizuizini Nchini Algeria tangu Agosti 30, 2021.
Mbali na kushikiliwa wawili hao, imeelezwa kuwa mtu aliyewasaidia Viongozi hao kuvuka mpaka huo bila vibali ameshakamatwa na Polisi.
Kumekuwepo la wimbi la zuio la kusafiri na vifungo vya nyumbani dhidi ya Viongozi mbalimbali Nchini humo tangu Rais Saied alipovunja Bunge na kumfuta kazi Waziri Mkuu mwezi Julai mwaka huu
Chanzo: www.tanzaniaweb.live