Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tume ya Uchaguzi Kenya yasitisha uandikishaji wapiga kura kwa kukosa pesa

Chebukati IEBC yafunga zoezi la kuwasajili wapiga kura Kenya

Tue, 2 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imetupilia mbali agizo la mahakama la kuongeza muda wa zoezi la kuwasajili wapigakura kwa wiki moja.

Mnamo Jumanne, Novemba 1, IEBC ilisema kuwa itafunga leo zoezi la kuwasajili wapiga kura ambalo limekuwa likiendelea kwa muda wa mwezi mmoja. Tume hiyo ilibaini kuwa ilikuwa na uhaba wa kifedha na hivyo basi haiwezi kuendeleza zoezi hilo.

Awali, Mahakama kuu mjini Eldoret ilitoa agizo la kuendelea kusajiliwa kwa wapoiga kura ikisubiri kusikizwa kwa kesi iliyowasilishwa na mpiga kura kutoka kaunti ya Uasin Gishu.

Mahakama kuu mjini Eldoret ilitoa agizo hilo ikisubiri kusikizwa kwa kesi iliyowasilishwa na mpiga kura kutoka kaunti ya Uasin Gishu.

Jaji Eric Ogolla, katika uamuzi wake, aliagiza kwamba zoezi hilo lililotarajiwa kukamilika Jumanne, Novemba 2 baada ya muda wa siku 30, liendelee hadi Jumanne, Novemba 9, 2021.

Wiki jana IEBC ilitoa wito kwa Wakenya ambao bado walikuwa hawajajisajili kuchukua fursa ya wiki moja iliyosalia kufanya hivyo kwani haikuwa na mpango wa kuongeza muda.

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema tume hiyo ilitengewa Ksh1.2 bilioni kati ya KSh 4 bilioni ilizoomba kwa zoezi hilo.

“Baada ya Novemba 2, hatutakuwa na pesa za kuongeza muda wa kuandikisha wapigakura. Tume inaweza kumudu kufanya usajili wa watu wengi kwa siku 30 pekee,” Chebukati alisema.

Aidha alieleza kuwa tume hiyo ilihitaji KSh 1.3 bilioni za ziada kukagua sajili ya wapiga kura, na gharama zinginezo.

Chebukati alikuwa amefichua kuwa tume hiyo ilikuwa likilenga kusajili wapiga kura wapya milioni sita lakini katika muda wa mwezi mmoja, bodi ya uchaguzi haikukusanya vijana wa kutosha kushiriki katika zoezi hilo.

Bosi huyo wa IEBC aliambia Wabunge kuwa wanahitaji KSh 40 bilioni kuandaa uchaguzi 2022.

Hata hivyo, ombi hilo lilikataliwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti na Ugavi, Kanini Kega, ambaye alitaja bajeti hiyo kuwa kubwa na kutilia shaka IEBC kwa kupanga kununua karatasi za kupiga kura kwa bei ya juu.

Chebukati alitetea uamuzi wa IEBC kuhusu ununuzi wa karatasi za kupigia kura akisema kuwa itagharimu Ksh35 kununua karatasi moja ya kupigia kura kwa sababu ya vipengele vipya vya usalama.

Chebukati alitetea uamuzi wa IEBC kuhusu ununuzi wa karatasi za kupigia kura akisema kuwa katarasi moja itagharimu KSh 35 kununua kutokana na vipengele vya usalama.

Mwenyekiti wa IEBC aliteta zaidi kuwa bodi hiyo ya uchaguzi imeamua kununua katarasi hizo kwa ajili ya kutoaminiana baina ya maafisa wa tume yake.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke