Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tuju adaiwa kuahidi IEBC vinono wakimtangaza Odinga mshindi

TUJU 1.png Tuju adaiwa kuahidi IEBC vinono wakimtangaza Odinga mshindi

Mon, 29 Aug 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mengi yanazidi kuibuka kuhusu yaliyokuwa yakiendelea katika ukumbi wa Bomas kati ya Agosti 9 na Agosti 15.

Raphael Tuju anaripotiwa kuahidi IEBC zawadi wakikarabati matokeo ya urais. Bomas ndipo tue huru yta uchaguzi na mipaka nchini IEBC ilikuwa na kitu cha kitaifa kujumuisha kura za urais.

Sasa kamishna Abdi Guliye anasema aliyekuwa katibu wa Jubilee Raphael Tuju pamoja na Seneta Amos Wako walifika Bomas Agosti 15.

Alisema wawili hao walitaka makamishna kukoroga hesabu ili kumfaidi kiongozi wa Azimio Raila Odinga.

Tuju alidaiwa kutaka hesabu imtangaze Raila mshindi na iwapo hilo litakuwa ngumu, basi wahakikishe kuwa kuna duru ya pili.

"Alisema tukifanya hivyo kutakuwa na zawadi kubwa kwetu," hayo yanafichuka katika kiapo alichowasilisha mahakamani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live