Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tshisekedi 'alikubali kukutana na Kagame' – Angola

Tshisekedi 'alikubali Kukutana Na Kaga Tshisekedi 'alikubali kukutana na Kagame' – Angola

Wed, 28 Feb 2024 Chanzo: Bbc

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inasema kuwa Rais Félix Tshisekedi "amekubali kukutana na mwenzake wa Rwanda" katika mazungumzo yenye lengo la kusuluhisha vita mashariki mwa Kongo.

Katika mtandao wa kijamii wa X, ofisi ya rais wa Congo inarudia maneno ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Tete António:

"Rais Félix Tshisekedi amekubali kukutana na mwenzake wa Rwanda."

Serikali ya Rwanda na serikali ya Angola hazikuwa zimetangaza chochote rasmi.

Nchi mbalimbali ziliendelea kuwaomba viongozi wa nchi hizo wakutane na kujadili utatuzi wa mgogoro huo.

Mwishoni mwa mwaka jana alipokuwa akifanya kampeni, Tshisekedi alisema atazungumza tena na Kagame” tu mbele ya Mungu ambaye atatuhukumu sisi".

DRC ilisema hayo baada ya mkutano wa saa tatu siku ya Jumanne mjini Luanda, kwa mwaliko wa mpatanishi, Rais wa Angola, João Lourenço, ambaye ni mpatanishi katika mzozo huo.

Ofisi ya rais wa RD Congo inarudia maneno ya Waziri António akisema kwamba kitakachofuata ni kwamba utaratibu huo unafanya kazi katika ngazi nyingine kuhakikisha mkutano huo unafanyika.

Mwezi huu nchini Ethiopia, Lourenço alikuwa amekutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame na Tshisekedi, kila mmoja tofauti, kama ilivyoripotiwa na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo, kando na mkutano wa wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika.

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Kinshasa wiki iliyopita, Tshisekedi alisema kuwa mtu pekee ambaye anataka kuzungumza naye ni Rais Kagame, kwamba hawezi kwenda kwenye mazungumzo na kundi la waasi la M23.

Ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa (UN) na DRC wanaishitumu Rwanda kwa kusaidia harakati ya M23 dhidi ya serikali ya Kinshasa, mashtaka ambayo Rwanda imekuwa ikiyakanusha.

Serikali ya Rwanda na ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa pia inaishutumu Congo kwa kufanya kazi na kundi la waasi wa Rwanda wanaoendesha harakati zao mashariki mwa Congo (FDLR), ambao Rwanda inadai walihusika na mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 na wenye hila dhidi ya serikali ya Rwanda. DRC pia inakanusha madai hayo.

Chanzo: Bbc