Thu, 21 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Nigeria, Bola Tinubu ataweka marufuku ya miezi mitatu kwa mawaziri na maafisa wengine wa serikali kusafiri nje ya nchi kwa fedha za umma.
Mkuu wa Utawala, Ofisi ya Rais Tinubu amesema hatua hiyo imesbabishwa Rais kuwa na “wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa gharama za usafiri” kutokana na safari za maafisa wa serikali.
Marufuku hiyo itaanza Aprili 1. Rais Tinubu na utawala wake umeshutumiwa na baadhi ya watu kutokana na safari za mara kwa mara nje ya nchi.
Tangu alipoapishwa mwezi Mei 2023, Bwana Tinubu amefanya zaidi ya ziara 15 nje ya nchi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live