Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tanzia: Mwanasiasa Maarufu wa Murang'a PMG Kamau Afariki Dunia

Dc287880c2134709 Tanzia: Mwanasiasa Maarufu wa Murang'a PMG Kamau Afariki Dunia

Mon, 12 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wakazi wa Murang'a Jumapili Aprili 12 walipatwa na tanzia baada ya kumpoteza mwanasiasa PMG Kamau

- Mbunge wa Kandara Alice Wahome alimtaja PMG kama hasimu aliyemtambua vilivyo haswa ustadi wake kwenye mijadala

- Wakazi wa Mt Kenya wanamtambua sana PMG maarufu kama 'independent thinker' kutokana na mijadala yake kwenye runinga zinazopeperusha kwa Kikuyu

Mwanasiasa tajika wa kaunti ya Murang'a PKG Njuguna Kamau maarufu kama wa Ruth amefariki dunia.

Wa Ruth alikuwa maarufu kutoka na uchanganuzi wake wa siasa za Mlima Kenya na urithi wa Rais Uhuru Kenyatta ambazo amekuwa akifanya kwenye runinga ya Inooro.

PMG alikuwa kwenye ulingo wa siasa kuanzia 2012 ambapo aliwania ubunge wa Kandara lakini akapoteza.

2017 alijitosa tena na kupambana na Mbunge Alice Wahome ambaye alimpiku tena lakini umahiri wake ukatambulika.

Wahome alitaja kifo chake kama pigo kwa wakazi wa Kandara huku akimtambua kama kiongozi aliyekuwa stadi kwenye mijadala.

"Ni siku ya huzuni Kandara. Wingu la kifo limetuangukia. PMG Kamau aka Waruth alikuwa ni hasimu wa kutambulika aliyekuwa akipigania aliyoyataka kwa nguvu zake zote," alisema Wahome.



Alisema uwezo wa PMG kwenye mijadala ulikuwa usio kifani na atakumbukwa kama mtetezi wa wakazi wa Kandara.

"Natuma rambirambi zangu kwa familia yake, marafiki na wakazi wa Kandara. Pumzika pema," alisema kwenye Facebook.

Runinga ya Inooro pamoja na ile ya Kameme zilimuomboleza PMG na kusema mashabiki wao watamkosa mchanganuzi waliyempenda.

Alijulikana sana pia kwa kujitambua kama asiyeweza kushawishika kwa urahisi akisema yeye ni 'independent thinker'.

Aliwatetea wakazi wa Murang'a haswa kwenye suala la ardhi ya Del monte ambapo wakazi wamekuwa wakiteta kunyanyaswa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke