Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tanzia: Mwanahabari wa BBC Kate Mitchell afariki dunia

6b8bb40be61261bc Tanzia: Mwanahabari wa BBC Kate Mitchell afariki dunia

Sun, 21 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Maafisa wa upelelezi wameanzisha uchunguzi kufuatia kifo cha kutatanisha cha mwanahabari mkuu wa Shirika la Kimataifa la utangazaji la BBC Kate Mitchell.

Mwili wa mwanahabari Kate Mitchell ulipatikana katika chumba cha hoteli moja jijini Nairobi siku ya Ijumaa, Novemba 19. Mitchell alikuwa mwanahabari wa shirika la BBC na hadi kifo chake alikuwa akifanyia kazi nchini Ethiopia.

Kabla kifo chake Mitchell alikuwa amefanya kazi katika shirika hilo kwa muda wa miaka 14

Afisa mkuu wa polisi Augustine Ntumbi amethibitisha kwamba mwili wa Mitchell ulipatikana katika chumba cha hoteli moja jijini Nairobi siku ya Ijumaa, Novemba 19.

Shirika la BBC pia lilitangaza kifo cha Mitchell ambaye hadi dakika ya mwisho alikuwa akifanyia kazi yake nchini Ethiopia.

" Nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wetu Kate Mitchell. Alifariki dunia akiwa jijini Nairobi kwenye chumba cha hoteli," Sehemu ya tangazo hilo kama ilivyonukuliwa.

Shirika hilo lilisema bado halijabaini chanzo cha kifo cha Mitchell na kufutilia mbali madai kwamba huenda kilitokana na majukumu yake kama mwanahabari wa kimataifa.

" Chanzo cha kifo cha Kate hakijabaini lakini tunashirikiana na ubalozi wa Uingereza na polisi jijini Nairobi kufanya uchunguzi. Tutapeana usaidizi kadri ya uwezo wetu kwa wapepelezi na kile tunachokijua, hakuna ishara kwamba kifo chake kilitokana na majukumu yake kama mfanyakazi wa BBC," Taarifa zaidi ilisoma.

Kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Ethiopia, Mitchell aliwahi kufanya kazi nchini Sudan Kusini na Zambia.

Kwenye habari zingine sawa na hii, OCS wa kituo cha polisi cha Wanguru kaunti ya Kirinyaga, alipatikana nyumbani kwake akiwa amefariki dunia mapema Jumapili, Novemba 21.

Julius Mwangi Ndungu alifariki dunia baada ya polisi wenzake kukosa kupokea simu yake usiku wa Jumamosi, Novemba 20, inaonekana alihitaji usaidizi baada ya kulemewa na ugonjwa.

Polisi hao walienda nyumbani kwake mapema na kupata mlango ukiwa wazi walipoingia walikutana na mwili wake sebuleni ukiwa kwenye sakafu.

“Walifika nyumbani kwa OCS Julius Mwangi Ndung'u baada ya kumpigia simu nyingi lakini akakosa kupokea tangu Jumamosi asubuhi," ripoti ya kisa hicho ilisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke