Wed, 31 Mar 2021
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke
Mbunge wa Kiambaa Paul Koinange amefariki dunia.
Kifo cha Koinange kilitangazwa Jumatano asubuhi na inaripotiwa alifariki kutokana na makali ya covid-19.
Mbunge huyo alikuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi alipolazwa baada ya kuugua.
Rais Uhuru Kenyatta alituma jumbe zake za pole kwa familia ya Koinange na wakazi wa Kiambaa akitaja kifo hicho kama pigo kubwa.
"Mkono wa kifo tena umechukua kiongozi wetu. Alikuwa ni kiongozi ambaye alijihusisha na amani na maendeleo ya nchi yetu," Rais Kenyatta alisema.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke