Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tangazo la Jamaa Kutoka Mt Kenya Akitafuta Mpenzi Lawavunja Mbavu Wanamtandao

Aff52edd5878b3eb Tangazo la Jamaa Kutoka Mt Kenya Akitafuta Mpenzi Lawavunja Mbavu Wanamtandao

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Katika karne hii wengi hutumia simu au mitandao kupenya roho za wale wanatamani kuwachumbia

- Jamaa mmoja kutoka eneo la Mlima aliamua kutumia mabango yaliyotundikwa kijijini akitangaza kuwa upweke umemtafuna siku nyingi

- Aliweka masharti ya kipusa anayemtafuta ikiwemo awe na watoto wawili na pia stadi wa kukama ng'ombe

Jamaa mmoja kutoka eneo la Mt Kenya amewavunja mbavu wanamtandao baada ya kuchapisha tangazo la kumtafuta mchumba.

Kupitia kwa bango, ndume huyo alielezea matamanio ya roho yake na kumtaka kipusa yeyote mwenye kiu cha penzi kutuma maombi.

"Kipusa yeyote mwenye haja ya kuolewa mradi awe na miaka thelathini au thelathini na tano," bango hilo lilielezea.

Licha ya kuwa wanaume wengi huhofia kuingia kwenye ndoa na wapenzi walio na watoto tayari, ndume huyo alisema yeye hilo ndilo anataka.

Kando na kuwa ametimiza sharti la miaka, mpenzi alitakikana awe amejifungua angalau watoto wawili.

"Awe na watoto wawili wasiozidi umri wa miaka miwili," tangazo hilo la mchumba lilielezea zaidi.

Ilikuwa wazi pia kuwa atakayefanikiwa kuyeyusha roho ya bingwa huyo atajipata mashambani kwani inatakiwa ajue masuala ya mifugo.



"Awe ni stadi wa kukama ng'ombe," jamaa huyo alisema kwenye tangazo hilo lake.

Wanamtandao walivunjwa mbavu na tangazo hilo wakishangaa ni vipi jamaa aliamua kuandika mabango barabarani ya kutafuta uchumba.

Ilikuwa wazi kuwa mwanaume huyo amekuwa mpweke kwa muda na kuamua kutumia njia hiyo ya kuandika mabango na kuweka nambari yake ya simu ili mwenye kiu kumtafuta.

Suala la mapenzi huwazungusha wengi na hata kuwa vigumu kwa wanaume kuwarushia kina dada chambo cha kuteka roho zao.

Kwa wengine, kuyeyusha roho za kina dada kiasi cha kutikisa mayai ya uzazi huwa kama kufumba na kufumbua.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke