Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Taasisi ya Tony Blair yamteua aliyekuwa waziri Balala kuwa mshauri

Taasisi Ya Tony Blair Yamteua Aliyekuwa Waziri Balala Kuwa Mshauri Taasisi ya Tony Blair yamteua aliyekuwa waziri Balala kuwa mshauri

Fri, 6 Oct 2023 Chanzo: Radio Jambo

Aliyekuwa waziri wa Utalii, Wanyamapori na Urithi Najib Balala ameteuliwa na Taasisi yaTony Blair for Global Change (TBI) kuwa Mshauri wa Utalii.

Waziri huyo wa zamani alisema atakuwa sehemu ya timu ya kimataifa ya wana mikakati, wataalamu wa sera, na watendaji wa utoaji ambao watafanya kazi na viongozi wa kisiasa na serikali kuleta mabadiliko duniani kote.

"Nimeheshimiwa kuteuliwa na Taasisi ya Tony Blair for global change (TBI) kama Mshauri wa Utalii sehemu ya timu ya kimataifa ya wana mikakati ya kisiasa, wataalam wa sera, na watendaji wa utoaji ambao hufanya kazi na serikali na viongozi wa kisiasa duniani kote kuleta mabadiliko, Waziri wa zamani alisema katika taarifa.

Jukumu kuu la Balala kama mshauri wa utalii wa TBI litaanzia kutoa ushauri kwa taasisi hiyo kuhusu mikakati, sera na programu za utalii.

Taasisi ya Tony Blair (TBI) ni shirika la kimataifa lililoanzishwa na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.

Tony Blair aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza kati ya 1997 na 2007. Alikuwa kiongozi wa Chama cha Labour kuanzia 1994 hadi 2007 na alianzisha Taasisi ya Tony Blair mnamo Desemba 1, 2016.

Chanzo: Radio Jambo