Fri, 8 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
José Eduardo dos Santos aliyeongoza Angola kwa takriban miaka 40, kuanzia mwaka 1979 - 2017 amefariki dunia akiwa na miaka 79
Taarifa ya kifo chake zimethibitishwa na Serikali ya Angola, ikielezwa amefariki akiwa Hospitalini Barcelona Nchini Uhispania kutokana na maradhi ambayo hayajawekwa wazi
Kiongozi wa Taifa hilo, Joao Lourenco ametangaza siku tano za maombolezo kuanzia leo Julai 8, 2022 na Bendera ya Nchi itapepea nusu mlingoti
Chanzo: www.tanzaniaweb.live