Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sudan: Kiongozi wa RSF atuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita

Mkuu Wa RSF Atoa Wito Kwa Jumuiya Ya Kimataifa Kuingilia Kati Sudan: Kiongozi wa RSF atuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita

Tue, 9 Jan 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiongozi wa kikosi cha wanamgambo nchini Sudan cha RSF Mohamed Hamdan Daglo anatuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita nchini Sudan, wakati huu akiendeleza ziara yake kwa mataifa ya Kikanda, ziara inayondekana kuwagawa msimamo ya viongozi wa kikanda.

Hamdan Daglo amekua akifanya safari za kikanda ikiwa ni juhudi za kujaribu kujaribu kutafuta ungwaji mkono na viongozi wa kikanda na bara Afrika, kujaribu kusuluhisha mzozo ambao umepelekea vita kati ya kikosi chake cha RSF na jeshi la Sudan.

Kiongozi huyo wa RSF pia alizuru Afrika Kusini ambapo alikutana na rais Cyril Ramaphosa

Hamdan amefanya mazungmzo na marais wa Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Rwanda, na Djibouti pamoja na Ethiopia, ili kutafta njia mwafaka ya kumaliza mzozo na kwamba mchakato wa amani unaoendelezwa na IGAD, unastahili kufikia suluhu ya kisiasa itakayoleta amani ya kudumu nchini humo, ambapo kiongozi huyo anapata ungwaji mkono kutoka utawala wa Chad.

Naye kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Sudan Abdel Fattah Al-Burhan akionekana kupata ungwaji mkono kutoka kwa Misri na Eritrea.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live