Thu, 4 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Spika wa zamani wa Afrika Kusini Nosiviwe Mapisa-Nqakula ameshtakiwa na makosa 12 ya ufisadi na moja la utakatishaji fedha.
Alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza siku ya Alhamisi baada ya kujisalimisha polisi saa za asubuhi.
Mwanasiasa hyo anatuhumiwa kwa kudai rushwa ili atoe mikataba wakati akiwa waziri wa ulinzi.
Alikanusha kufanya makosa yoyote mahakamani akisema: “Sina tabia ya kufanya uhalifu.”
Lakini mwendesha mashtaka Bheki Manyati ameiambia mahakama ya mwanzo ya Pretoria kuwa kuna “ushahidi wa kutosha” dhidi ya Bi Mapisa-Nqakula.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live