Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Spika Muturi atangaza atawania urais ifikapo 2022 kumrithi Uhuru

2baf3ca0fcdd3783 Spika Muturi atangaza atawania urais ifikapo 2022 kumrithi Uhuru

Sun, 4 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Muturi Jumamosi Julai 3 aliwataka wakazi wa Mbeere wakiongozwa na watumishi wa Bwnaa kumuombea kukubalika katika safari ya kuingia IkuluAlisema ana tajriba ya kutosha kuliongoza taifa baada ya Rais Uhuru kustaafu 2022Spika huyo alisema kuna vigogo wamekuwa wakitaka awe mgombea mwenza wao lakini amedinda kwa sababu anataka aingie Ikulu na kuleta mageuziSpika wa Bunge Justin Muturi amesema anatosha kuingia katika viatu vya Rais Uhuru Kenyatta ifikapo 2022.

Muturi ambaye hivi karibuni alitawazwa kuwa msemaji wa jamii za Gikuyu, Embu na Meru alisema atawania urais akisema kuongoza taifa la Kenya itakuwa kazi rahisi kwake.

Akiongea nyumbani kwake Mbeere katunti ya Embu, Muturi aliwataka wakazi kumuunga mkono akisema wakifanya hivyo atakuwa na nguvu ya kutafuta ufuasi sehemu zingine za taifa.

"Ninajua vizuri kuwa mkikubali kuniunga mkono na kuniombea, basi itakuwa rahisi kwangu kuingia Ikulu," aliwaambia viongozi wa kanisa.

Mwanasiasa huyo hata hivyo hakufichua chama atakachotumia kuingia Ikulu huku akisema kuna baadhi ya vigogo ambao wanataka awe mgombea mwenza wao lakini amedinda.

Alisema ana mpango kabambe wa jinsi anataka kuongoza Kenya na hilo litakamilika tu iwapo ni yeye atakuwa Ikulu.

"Niko na ndoto ya nchi ambayo itaongozwa kupitia nidhamu na mimi ndiye mtu atakayefanya hivyo. Huwezi kufanya hivyo ukiwa nambari mbili," Muturi alisema.

Alisema treini yake imeondoka na sasa mpango wake ni kuzuru kila eneo nchini ili kutafuta uungwaji mkono.

Muturi alianzisha safari yake kwa kutawazwa msemaji wa jamii ya Gikuyu katika eneo la Mukuru wa Nyagathanga.

Viongozi wengine wa Mlima walikashifu hatua yake ya kuingia kwenye eneo hilo wakisema ni mahali takatifu ambapo hapafai kuingizwa siasa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke