Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sossion ataja sababu ya kulia wakati akitangaza kujiuzulu:

C9c24aac90924ab5 Sossion ataja sababu ya kulia wakati akitangaza kujiuzulu:

Thu, 8 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wilson Sossion alianza kazi yake ya ualimu akifunza kemia na kilimo katika Shule ya Upili ya Tenwek Kaunti ya BometMbunge huyo aliyeteuliwa na ODM aliidhinishwa kwanza na waalimu mnamo 1999 kwa nafasi ya katibu mtendaji wa KNUT katika wilaya ya zamani ya Bomet lakini akashindwaAlijiuzulu wadhifa wake wa Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Kenya (Knut) Ijumaa, Juni 25Katibu Mkuu wa zamani wa Muungano wa Walimu nchini (KNUT) Wilson Sossion ametaja sababu ya kulia wakati akijiuzulu Ijumaa, Juni 25.

Akizungumza na Daily Nation Jumanne, Julai 6, Sossion alisema kuwa alianza kulia baada ya kuwataja walimu wa Bomet ambao walimtoa darasani ili kulainisha sekta ya elimu nchini.

Tafakari kuhusu alipoanziaSossion ambaye alitafakari juu ya mwanzo wake akiwa mwalimu katika Shule ya Upili ya Tenwek katika Kaunti ya Bomet alisema kwamba wakati wowote hakuwahi kufikiria kwamba angeweza kufikia uongozi wangazi ya juu zaidi KNUT.

"Wakati nilitafakari juu ya nyakati hizo za wale walimu kuja kwangu na kunipa msaada wa hali ya juu wa kisiasa licha ya upinzani wa serikali ilitosha kwangu kutoa machozi ya furaha kwa hivyo machozi hayo hayakuwa ya uchungu, yalitakiwa kwa ajili ya walimu wa Bomet," Sossion alielezea.

Alisema kuwa ikiwa wenzake wa zamani hawangeweza kumchukua, basi angekuwa bado yupo darasani akifundisha katika moja ya shule zilizo ndani ya Bomet.

''Na ikiwa singechaguliwa kuhudumu katika ofisi ya KNUT, walimu wa Kenya wasingeniona. Kwa hivyo, waalimu wa Kenya walinitambua na kunichagua niende Nairobi mnamo 2007 na hapo ndipo nilipopata jukwaa la kitaifa ambalo naamini nilifanya bidii," Sossion alisema na kuongeza kuwa ilibidi ajiuzulu kwa sababu wakati wake kutoka ofisini alikuwa umefika.

Mwanaharakati mzito wa KNUTSossion alisema kuwa mbali na kuwa mwalimu pia alikuwa mwanaharakati mzito sana wa KNUT.

'' Ningeondoka tu shule mwishoni mwa mwezi kwa ajili ya kuchukua mshahara wangu. Hiyo ndiyo siku pekee ambayo nilikosekana shuleni. Nilifanya kazi shuleni kote na kazi yangu ilikuwa ya mfano mzuri katika siku ya tuzo za wilaya kila wakati nilikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliopata A ambayo iko katika Kemia na Kilimo lakini kwa kweli Kilimo nilikuwa na ya juu zaidi ikifuatiwa na Kemia," alielezea.

Mbunge wa ODM aliyeteuliwaMbunge huyo aliyeteuliwa kwa tikiti ya chama cha Orange Democratic Movement (ODM) pia alikuwa mwalimu wa mchezo wa kuigiza na mwalimu wa muziki ambaye kulingana naye alishika ngazi ya wilaya.

Kwanza aliidhinishwa na walimu mnamo 1999 kwa nafasi ya katibu mtendaji wa KNUT wilayani Bomet lakini akashindwa.

"Lakini nilichaguliwa kwa idadi kubwa ya kura mnamo 2000 na mnamo 2006 walimu wa Bomet walijitokeza kwa wingi kuhakikisha kuwa nilichaguliwa. Hao ndio watu ambao walionitoa darasani kuja kuboresha mfumo wa elimu nchini," Sossion alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke