Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sonko amzawadi mwanawe wa kuasili gari la kifahari baada ya kufuzu KCSE 2020

6deadab2fe3b74cd Sonko amzawadi mwanawe wa kuasili gari la kifahari baada ya kufuzu KCSE 2020

Thu, 13 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mtoto wa kupanga wa Gavana wa zamani wa Nairobi Mike Sonko, Gift Osinya alipata gredi ya B- kwenye mtihani wa KCSE 2020

- Kisha kiongozi huyo mkwasi alimzawadi gari maridadi aina ya Mercedes Benz kwa kupata gredi nzuri

- Mama yake alipakia video kwenye Instagram akianika gari jipya la Osinya

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko amewaacha wengi vinywa wazi baada ya kumzawadi mwanawe wa kupanga Moses Gift Osinya gari jipya la Mercedes Benz kama zawadi ya kupita mtihani wa KCSE.

Mvulana huyo ambaye aliasiliwa na kiongozi huyo tajiri baada ya mama yake kuawa kwenye shambulizi la kigaidi kanisani, alipata alama ya B- kwenye mtihani wa KCSE 2020.

Gift, ambaye pia alihojiwa na kituo kimoja nchini, alishikilia kwamba licha ya yale aliyopitia akiwa mtoto, ana ari ya kufuzu masomoni.

Huu ndio ujumbe wa mama yake Primrose Mbuvi kwenye ukurasa wake wa Instagram: "Tunajivunia"

Gift anaonyeshwa akiwa ndani ya gari hilo pamoja na ripota ambaye anazungumza kwenye kamera.

Punde anapomaliza kuripoti, kijana huyo aliwasha gari hilo maridadi na kuondoka kwenye makazi yao ya kifahari.

Maoni ya wanamtandao:

@nimpher_nimpher: "Matendo ya ukarimu Mungu akubariki."

@delvine_njheh_riy: "Mungu akubariki Mrs Mbuvi."

@ericthongori: "Endelea kuwa mama mwema kwa wanao. Mungu akubariki kwa moyo wako mkubwa, Mama Primrose."

@joycemoses583: "Mungu akubariki mama"

@mbithe724: "Mungu akubariki mama umefanya ya kutosha. Kongole kwake."

Sonko alilelezea furaha yake mitandaoni baada ya mwanawe wa kupanga Gift Osinya kuibuka miongoni mwa watahiniwa bora katika mtihani wa KCSE mwaka wa 2020.

Familia ya Sonko ilitangaza kwamba Osinya alipata gredi ya B- pindi matokeo yalipotolewa na Waziri wa Elimu George Magoha na wana furaha atajiunga na Chuo Kikuu kusomea kozi apendayo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke