Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sonko adai amefilisika, ataka korti imrejeshee dhamana yake ya KSh 15 milioni

Daa9f7281af6873d Sonko adai amefilisika, ataka korti imrejeshee dhamana yake ya KSh 15 milioni

Tue, 14 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike sonko amedai kwamba amefilisika na anataka korti imrejeshee pesa zake KSh 15 milioni ambazo alilipa kama dhamana wakati alikamatwa mwaka wa 2019.

Mike Sonko amesema alilipa KSh 15 milioni kortini kama dhamana kabla ya kuachiliwa huru Jumanne, Disemba 11, 2019Akiwasilisha ombi lake kwenye mahakama kuu, Sonko alisema kwa sasa hawezi akakimu mahitaji ya familia yake kwa sababu akaunti zake za benki zilifungwa.

Sonko alidai kwa sasa amefilisika na hana mahali pengine pa kupata fedha za kukimu familia

Sonko alisema alilipa pesa hizo Jumatano, Disemba 2019 kama dhamana ili awachiliwe baada ya kukamatwa kuhusiana na madai ya ufisadi.

Kwenye ombi lake alilolituma kortini, Sonko alisema kwa sasa amefilisika na hawezi kimu mahitaji ya familia yake.

Vile vile, Sonko alisema kwamba akaunti zake zote za benki zimefungwa na kwa hivyo maisha yameanza kuwa magumu kwa sababu hana mahali pengine pa kupata pesa.

Kupitia kwa wakili wake Philip Kaingu, Sonko alisema korti iko huru kuchukua baadhi ya mali yake anayomiliki ili ishikilie kama dhamana lakini imrudishie pesa hizo KSh 15 milioni.



" Ningependa korti inirejeshea KSh 15 milioni nilizolipa kama dhamana ili niweza kugharamia afya yangu, nilipe karo ya shule ya watoto, nilipe mawakili wangu na pia nikimu mahitaji ya familia yangu," Sonko alisema.

Sonko alisisitiza kwana hana mahali pengine pa kupata pesa za kulisha familia ikizingatiwa iko kubwa.

Aidha, Sonko aliongezea kwamba ana magari ya kifahari yanayogharimu zaidi ya KSh 30.4 milioni na alisema yuko tayari kuyapatiana kwa korti ili arejeshewa pesa zake KSh 15 milioni.

Awali kama ilivyoripotiwa na TUKO.co.ke, Sonko alikamatwa Ijumaa, Disemba 2019 baada ya mkurugenzi mkuu wa mashtaka Noordin Haji kutoa amri ya kukamatwa kwake kufuatia tuhuma za ufisadi.

Kabla ya kuamru kukamatwa kwa Sonko, Haji alikuwa amekusanya ushahidi wa kutosha kuhusu jinsi gavana huyo na baadhi ya viongozi katika serikali yake walivyofyonza fedha za umma.

Akaunt tisa za Sonko ikiwemo na Diamond Trust Bank, National Bank na Equity zilifungwa baada ya Hakimu mkuu E. Riany kutoa amri Disemba 11, 2019.



Siku chache baadaye, Sonko aliachiliwa huru na Hakumu Mkuu Douglas Ogoti kwa dhamana ya KSh 15 milioni au bondi ya KSh 30 milioni.

Sonko alitimuliwa uongozini na mawakilishi wa wadi wa bunge la kaunti ya Nairobi kwa kile walichokitaja kuwa matumizi mabaya ya afisi.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke