Sat, 23 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu sita wameuawa katika mlipuko uliotokea katika mgahawa Jijini Mogadishu ambao ulikuwa ukitumiwa na askari Polisi na Wabunge, Ijumaa Aprili 22, 2022
“Watu wengine saba wamejeruhiwa kutokana na mlipuo huo,” amesema Abdikadir Abdirahman, Mkuu wa Gari la Wagonjwa.
Aidha, mteja aliyekuwa eneo la tukio alisema kulisikika milio ya risasi kadhaa lakini hajui hasa nini kilikuwa nyuma ya pazia
Polisi hawajasema ukubwa wa madhara kwa jumla ya mlipuko huo lakini wanaamini bomu lilitupwa ndani ya mgahawa na hakuna mbunge ambaye alipoteza maisha katika tukio hilo
Chanzo: www.tanzaniaweb.live