Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sintofahamu baada ya mwili wa mtoto wa miezi 7 kutoweka katika makafani

A05930a94a56e4f5 Sintofahamu baada ya mwili wa mtoto wa miezi 7 kutoweka katika makafani

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Princess Wambui aliaga dunia kutokana na homa ya mapafu Alhamisi, Julai 29 akipokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya Kerugoya Familia yake ilikuwa imeenda kuchukua mwili Ijumaa, Julai 30 wakati waliarifiwa kuwa maiti ya mwanao haiopoMazishi ya Wambui yalipangwa kufanyika katika kijiji cha Kiangungu Familia ya mtoto wa miezi saba inatishia kuishtaki hospitali ya rufaa ya Kerugoya, kufuatia kutoweka kwa maiti ya mwanao katika makafani ya hospitali hiyo.

Msichana huyo kwa jina Princess Wambui aliaga dunia kutokana na homa ya mapafu Alhamisi, Julai 29 wiki iliyopita wakati akipokea matibabu katika hospitali hiyo ya rufaa.

Familia yake ilikuwa imekwenda kuchukua mwili Ijumaa, Julai 30 walipoarifiwa na mmoja wa wahudumu katika makafani hiyo kwamba mwili huo ulikuwa umetoweka na kisha akaondoka.

Mazishi ya Wambui yalipangwa kufanyika katika kijiji cha Kiangungu.

Daily Nation iliripoti kuwa, familia ya marehemu iliwalaumu wahudumu wa makafani hiyo pamoja na uongozi wa hospitali kwa utepetevu kazini huku mamake mtoto huyo Purity Wangari akiapa kuwa atafanya kila jambo kuupata mwili wa bintiye.

Read also

Mumewe Caroline Kangogo Aomba Kutowahutubia Waombolezaji

"Sikuamini wakati waliniambia mwili wa binti yangu haupo. Mhudumu na usimamizi wa hospitali wanapaswa kutuelezea ni wapi walipeleka mwili,” Miss Wangari alilia.

Kwingineno, TUKO.co.ke iliripoti kuwa familia moja mtaani Kayole, Nairobi ilikuwa ikiomboleza kifo cha jamaa yao ambaye aliaga dunia katika hali ya kutatanisha wiki mbili baada ya kulazwa katika Hospitali ya Mama Lucy.

Jane Kari alilazwa mnamo Julai 12, 2021, na mumewe, Naftaly alipokea simu kutoka kwa kituo hicho ikimjulisha kwamba alikuwa amehamishiwa hadi hospitali ya Mbagathi kutokana na dalili za COVID-19.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke