Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shujaa wa filamu ya "Hotel Rwanda" akamatwa kwa ugaidi

A 40 660x400 Shujaa wa filamu ya "Hotel Rwanda" akamatwa kwa ugaidi

Tue, 1 Sep 2020 Chanzo: millardayo.com

Leo September 1, 2020 Taarifa kutokea nchini Rwanda zinasema Paul Rudesabagina ambaye aliwasaidia Wanyarwanda wengi wakati wa Mauaji ya Kimbari kwa kuwahifadhi kwenye Hoteli aliyokuwa anaiongoza amekamatwa.

Ujasiri wake ulisababisha kutengenezwa kwa filamu inayoelezea kisa hicho inayofahamika kwa jina la ‘Hotel Rwanda’.

Paul anatuhumiwa kwa mashtaka mbalimbali yanayohusiana na makosa ya ugaidi, Mamlaka za Uchunguzi Nchini Rwanda zimeeleza kuwa wamefanikiwa kumkamata Rusesabagina kwa kushirikiana na mataifa mengine bila kuyaweka wazi.

Kwa nyakati tofauti, Paul Rusesabagina amekuwa akiikosoa Serikali ya Rais Kagame kwa jinsi ilivyomaliza mgogoro uliopelekea mauaji ya mwaka 1994.

LIVE: RAIS MAGUFULI “MLIPIGA MTI MBUNGE, ALIKUWA ANAUMWA”

Chanzo: millardayo.com