Wazima moto nchini Somalia wamekuwa wakishirikiana na polisi na raia katika juhudi za kuuzima moto mkubwa ambao umezuka mapema Jumapili katika soko la Bakara mjini Mogadishu.
Moto huo mkubwa unaoripotiwa kuanza mapema asubuhi, umeteketeza maduka kwenye soko hilo kubwa kabisa mjini Mogadishu ambalo ni mashuhuri kwa wafanyibiashara wa bidhaa mbali mbali na wanunuzi.
Wengi waliofika kuanza shughuli zao za mwanzo wa wiki baada ya mapumziko ya wikendi, walipatwa na mshtuko kuuona moto ukisambaa kwa haraka.
Polisi nchini humo wamesema kwamba pindi tu, moto utakapo dhibitiwa, uchunguzi kujuwa chanzo cha moto huo utaanzishwa mara moja.