Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sheikh aomba msaada wa dharula vifo vya watu 100

Ap22303274915886 Custom D5f7ee23e13ca91b009243de9894fbf43aa0d9ce S1100 C50 1100x640 Sheikh aomba msaada wa dharula vifo vya watu 100

Mon, 31 Oct 2022 Chanzo: Dar24

Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud ametoa ombi la dharura la kutaka msaada wa kimataifa kwa wahanga waliojeruhiwa katika milipuko ya mabomu ya magari mwishoni mwa juma, ambayo yaligharimu maisha ya watu 100.

Maombi hayo ya Serikali, ni yale ya kuchangia damu huku makumi ya watu wakikusanyika nje ya hospitali katika mji mkuu wa Mogadishu, kutafuta habari za wanafamilia wao.

Jumamosi Oktoba 29, 2022 magari mawili yaliyokuwa yamejaza vilipuzi yalilipua dakika kadhaa karibu na makutano ya Zobe yenye shughuli nyingi, na kufuatiwa na milio ya risasi katika shambulio lililolenga Ofisi za Wizara ya Elimu ya Somalia.

Shambulio jingine kama hilo, lilitokea katika makutano yale yaliyokuwa na shughuli nyingi ambapo lori lililokuwa na vilipuzi lililipuliwa Oktoba 14, 2017 na kuua watu 512 na kujeruhi zaidi ya 290, tukio ambalo lilikuwa ni baya zaidi kuwahi kutokea katika nchi hiyo yenye machafuko.

Kundi la Al-Shabaab, lenye mafungamano na Al-Qaeda limedai kuhusika na mashambulizi hayo, likisema wapiganaji wake walikuwa wakilenga Ofisi za Wizara ya elimu pekee.

Kufuatia hatua hiyo, Ikulu ya White House ya jijini Newy York nchini Marekani, ililaani shambulio hilo baya la kigaidi huko Mogadishu na kusema wahusika wanapaswa kuchukuliwa hatua kali.

Chanzo: Dar24