Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shambulizi la kivita laua 30 Congo

Shambuliziii Congoooo.png Shambulizi la kivita laua 30 Congo

Tue, 12 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Takriban watu 30 wameuawa katika siku mbili za mashambulizi ya watu wenye silaha mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Shirika la Msalaba Mwekundu limesema.

Ilitokea katika jimbo la Ituri, ambalo pamoja na jirani ya Kivu Kaskazini, wako chini ya hali rasmi ya kuzingirwa katika juhudi za serikali kukomesha mashambulizi ya makumi ya makundi yenye silaha.

Mashambulizi hayo yanakisiwa kutekelezwa na Allied Democratic Front (ADF), mojawapo ya makundi mabaya zaidi ya waasi wanaoendesha shughuli zao katika eneo hilo.

Walifanya vitendo vya kikatili - baadhi ya waathiriwa walikutwa wakiwa wamefungwa - wengine walikuwa wamekatwa koo.

Nyumba zilichomwa na mali kuporwa. Mwezi Disemba, zaidi ya wanajeshi 1,000 wa Uganda walivuka na kuingia DR Congo kwa kile kilichokusudiwa kuwa operesheni ya pamoja ya kijeshi kuwashinda ADF.

Lakini licha ya kuahidiwa maendeleo, kundi hilo limeendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara kwa jamii zilizo hatarini.

Huko Kivu Kaskazini, kundi lingine la waasi linaloitwa M23 hivi karibuni limeanzisha upya uasi unaoviteka vijiji vinavyoongeza mzozo wa usalama.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live