NAIROBI, Kenya. Kundi la kigaidi la Al Shabab limejinadi kufanya shambulio katika kambi ya kijeshi nchini Kenya inayotumiwa na wanajeshi wa Kenya na Marekani.
Katika taarifa yake kundi hilo lilijinadi kufanya shambulio hilo katika kambi hiyo iliyokuwa Kusini Mashariki mwa Kenya lakini taarifa zinadai kwamba shambulio hilo lilidhibitiwa.
“Kuna shambulio limefanywa lakini limedhibitiwa,'' alisema Irungu Macharia, ofisa wa Serikali mjini Lamu ilipo kambi hiyo. Hata hivyo Macharia hakusema kama kuna madhara yoyote ya kibinadamu au uharibifu wa mali uliotokea.
Katika taarifa ya Jeshi la Ulinzi la Kenya ilielezwa kwamba magaidi wanne waliuawa na kwamba mpango wa magaidi hao haukufanikiwa.
Taarifa ya kambi ya kijeshi ya Marekani barani Afrika ilieleza kulijua tukio hilo lakini taarifa hiyo haikueleza kwa mapana undani wa tukio zima.
Al Shabab ni kundi la kigaidi linalosifika kwa kufanya mashambulizi ya kigaidi maeneo mbalimbali hasa kwa Marekani na washirika wake duniani kote