Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shaffie Weru na Kikosi Chake Wafutwa Kazi HomeBoyz Redio

43593fc6a9965d99 Shaffie Weru na Kikosi Chake Wafutwa Kazi HomeBoyz Redio

Sun, 28 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Watangazaji wa kipindi cha asubuhi katika redio ya HomeBoyz Shaffie Weru, Joseph Munoru almaarufu DJ Mfalme na Neville Muysa wamefutwa kazi.

Watatu hao walitimuliwa baada ya kutoa matamshi ya kudhalilisha mwanamke walipokuwa wakijadili unyanyasaji wa kijinsia.

Kupitia taarifa, kampuni ya Radio Africa Group ambayo inamiliki redio ya HomeBoyz ilisema hatua hiyo imechukuliwa baada ya uchunguzi kuhusu matamshi hayo.

Watatu hao wanaripotiwa kusema maneno yaliyoonekana kuunga mkono unyanyasaji wakijinsia kwenye kipindi chao Alhamisi Machi 24 wakati wa kipindi cha Lit Off.

"Wamefutwa kazi baada ya uchunguzi kamili kuhusu waliyoyasema Alhamisi ambapo baadaye walisimamishwa kazi. Washika dau na waskilizaji watakubali hatua hii kwa sasa ndiyo inafaa kuchukuliwa," taarifa cha usimamizi wa kituo hicho ilisema.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa kampuni haikuwa imetoa ruhusa kwa watatu hao kujadili mada waliyoamua kuizungumzia.

"Jumbe walizozisema hazikuwa zimeruhusiwa wala kujadiliwa na uongozi wa kampuni kabla ya kujadiliwa hewani," taarifa hiyo iliongeza.



Kampuni hiyo iliongeza kuwa ina sheria zake za uhariri na yale ambayo yanafaa kuzungumziwa na wafanyikazi wake.

Walisema ni jukumu la kila mfanyikazi kuhakikisha taarifa au jumbe anazotoa haziungi mkono unyanyasaji wa aina yoyote.

Kwenye kipindi hicho, wanadaiwa kusema kuwa kipusa Eunice Wangari alifaa kupokea yale alipata kutoka kwa mpenziwe awalipokosana.

Wangari aliripotiwa kutupwa kutoka nyumba alipokuwa na mpenzi wake baada ya tofauti kuibuka kati yao.

Maneno ya watangazaji hao yalikashifiwa na wengi yakidaiwa kuunga mkono dhuluma wanazofanyiwa wanawake.

Kampuni ya EABL ilikashifu hilo pia na kutangaza kuondoa matangazo yake ya kibiashara kutokana na hulka za watatu hao.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke