Thu, 23 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mamlaka ya Mawasiliano (CA) imetoa onyo hilo kwa Vituo 6 vya Luninga kwa kuonesha mubashara Maandamano ya Machi 20, 2023 yaliyolenga kuipinga Serikali yakiratibiwa na Kiongozi wa Azimio La Umoja, Raila Odinga.
Vituo husika ni Citizen TV, NTV, K24, KBC, TV47 na EbruTV ikielezwa vimekiuka Kanuni ya Utangazaji kwa kurusha matangazo ya Mikutano ya Hadhara
Mamlaka hiyo imesema kurushwa moja kwa moja kwa matangazo hayo ilikuwa ni aina ya uchochezi kwa Umma, na huenda ikavuruga Amani ya Nchi
Chanzo: www.tanzaniaweb.live