Tue, 28 May 2024
Chanzo: Bbc
Mafuruku ya matumizi ya muguka, aina ya miraa katika serikali za kaunti sio halali, amesema waziri wa kilimo Mithika Linturi, akieleza kuwa muguka ni zao lililoratibiwa kulingana na Sheria ya Mazao ya 2013 na kanuni za miraa 2023.
Hayo yanajiri baada ya Rais Ruto na uongozi wa Embu kufanya mkutano maalum Jumatatu kujadili kupigwa marufuku kwa muguka katika kaunti kadhaa.
Gavana Cecily Mbarire alikuwa miongoni mwa waliohudhuria mkutano wa Jumatatu katika Ikulu ya Nairobi, pamoja na naibu gavana, seneta, mwakilishi wa wanawake, na wabunge wote wa bunge la kaunti.
Chanzo: Bbc