Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yakubali kulipa Tsh. Bilioni 1.3 za waliosaidia kukamtwa magaidi

A544de1c677c90a9 Serikali yakubali kulipa Tsh. Bilioni 1.3 za waliosaidia kukamtwa magaidi

Mon, 22 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Hatimaye Serikali imesalimu amri na kukubali kutoa KSh60 milioni (zaidi ya tsh. bilioni 1) kama zawadi kwa watu waliosaidia kukamatwa kwa watuhumiwa watatu wa ugaidi waliotoroka Gereza la Kamiti kukamatwa baada ya kusukumiwa presa na umma.

Msemaji wa Polisi Bruno Shioso alithibitisha kuwa watu hao watapokea malipo yao kikamilifu. Hata hivyo, alionya kwamba lazima ukaguzi utafanywa kuainisha taarifa ya yule ambaye alisaidia watatu hao kukamatwa Shioso pia aliongezea kuwa majijna ya watakaofaidika na pesa hizo hayatachapishwa ili kulinda usalama wao

Katika taarifa siku ya Jumapili, Novemba 21, Msemaji wa Polisi Bruno Shioso alithibitisha kuwa watu hao watapokea malipo yao kikamilifu.

Hata hivyo, alionya kwamba lazima ukaguzi utafanywa kuainisha taarifa ya yule ambaye alisaidia watatu hao kukamatwa ambao walikuwa safarini kuelekea Somalia.

"Serikali inakiri kwamba kukamatwa tena kwa washukiwa hao kuliwezekana kwa kuungwa mkono na wananchi. Hakika taarifa za watu kadhaa ambao tofauti tofauti wanadai kuhusika katika ukamataji huo zimeripotiwa sana kwenye vyombo vya habari."

"Serikali inakusudia kuheshimu ahadi yake kwenye ofa ya zawadi ya pesa taslimu. Hii, hata hivyo, itazingatia mchakato wa uthibitishaji unaostahili ili kuhakikisha zawadi hiyo inaenda kwa wapokeaji wanaostahili," ilisoma taarifa hiyo kwa sehemu.

Shioso pia aliongezea kuwa majijna ya watakaofaidika na pesa hizo hayatachapishwa ili kulinda usalama wao.

Wakenya kadhaa wadai malipoWatu kadhaa wamekuwa wakijitokeza kwa vyombo vya habari wakidai wanastahili pesa hizo kwa kudokeza maafisa wa usalama kuhusu waliko watatu hao.

Musharraf Abdalla, Joseph Juma na Mohammed Abdi, waliripotiwa kuwa na nia ya kutorokea nchi jirani ya Somalia wakati walinaswa na wakazi na maafisa wa usalama katika eneo la Endau, Mwingi kaunti ya Kitui.

Mwanamume kwa jina Paul Mwaniki anaripotiwa kuongoza wanakijiji na maafisa wa polisi kuwakamata watatu hao.

Mwaniki aliomba serikali kutimiza ahadi yake kwa kumupa kama ilivyokuwa imeahidi.

Matiang'i arukaAwali, Tuko.co.ke iliripotia kwamba Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i Alhamsi alizungumzia kuhusu zawadi ambayo serikali ilikuwa imeahidi ya KSh 60M.

Waziri Matiangi ambaye alikuwa amefika Kamiti kushuhudia kurejeshwa kwa wafungwa hao hata hivyo alidinda kudhibitisha iwapo serikali itatekeleza ahadi yake.

"No...no...no, hatutaenda hiyo njia kwa sasa. Wacheni tusianze kushuku lolote wakati huu. Tutashughulikia hili kwa umakini mkubwa kama vile wenzangu wamesema,” Matiang’i alisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke