Polisi wa Afrika Kusini wanasema wamegundua miili 19 inayoshukiwa kuwa ya wachimba migodi haramu katika mji wa madini wa Krugersdorp magharibi mwa Johannesburg.
Polisi walisema katika taarifa siku ya Jumatano kwamba "wanaitikia wito kufuatia kugunduliwa" kwa miili hiyo katika mgodi mmoja unaoendelea katika eneo hilo.
Walisema uchunguzi wa awali ulipendekeza "marehemu walihamishwa na kuwekwa mahali walipogunduliwa".
Haijabainika jinsi watu hao wanaodaiwa kuwa wachimbaji haramu walikufa, ingawa polisi walisema hawakushuku mchezo wowote mchafu. Walisema uchunguzi wa maiti utafanywa ili kubaini chanzo cha kifo hicho.
Maelfu ya wachimbaji madini ambao hawajasajiliwa wanaendesha shughuli zao nchini humo kutafuta madini katika migodi ambayo haijatumika.