Thu, 14 Oct 2021
Chanzo: ippmedia.com
RAIS wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza kuongeza mishahara kwa walimu wa masomo ya sayansi na Tehama tu kwa madai ya kuwa wao ndio wanaochangia maendeleo ya jamii.
Rais Museveni amesema wangeweza kupandisha mishahara kwa walimu wote lakini uhaba wa fedha umelazimisha kuwapa kipaumbele walimu wanaohitajika zaidi.
Hatua hiyo imetajwa kwenda kinyume na makubaliano ya 2018 ambayo yanataka mishahara kupanda sawa kwa walimu wote.
Chanzo: ippmedia.com