Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Taliban yapiga marufuku wanawake kufanya kazi

Ebd552d82c71c9f7 Serikali ya Taliban yapiga marufuku wanawake kufanya kazi

Mon, 20 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wiki chache baada ya Taliban kunyakuwa mamlaka kutoka kwa Afghanistani, wanawake walioajiriwa na serikali jijini Kabul wamezuiliwa kufanya kazi hadi watakaposhauriwa kufanya hivyo.

Wiki moja iliyopita, serikali hiyo iliwazuia wanafunzi wa kike kuenda shuleni.

Wanawake wa Afghanistani ambao wamekuwa wakifanya kazi mjini Kabul wamepigwa marufuku kuendelea hadi watakaposhauriwa kufanya hivyoTangazo hilo linakujia mwezi mmoja baada ya Taliban kuchukuwa mamlaka kutoka kwa Afghanistan.

Taarifa hiyo ilitolewa na kaimu meya wa Kabul Hamdullah Namony, akielezea kuwa wanawake pekee ambao hawataguzwa ni wale ambao ajira zao wanaume hawawezi kuzifanya.

“Kuna kazi ambazo wanaume hawezi kufanya, tumewaomba wanawake kuzifanya hakuna njia nyingine," alitangaza.

Kazi ambazo wanaume hawawezi kufanya ni kusafisha vyoo, uhandisi na ubunifu.

Sheria za Kiislamu zenye itikadi kaliThe Guardian inaripoti kuwa kuwasitisha wanawake kufanya kazi ni inatokana na msimamo wa Taliban kutekeleza tamaduni za kiislamu.

Sheria hiyo mpya imekiuka ahadi ya serikali hiyo mpya kuwa uongozi wao utahakikisha kuwa haki za wanawake zitaheshimiwa.

Kumekua na sheria kadhaa ambazo zimekiuka haki ambazo wanawake wa Afghan wamekuwa nao, kwa mfano wiki moja iliyopita, serikali hiyo iliwazuia wanafunzi wa kike wa sekondari na msingi kuenda shuleni.

Isitoshe, wanafunzi wa kike katika vyuo vikuu walitengansia na wa kiume ili kuzingatia sheria za kiislamu kuhusu mavazi.

Tangazo hilo linajerejesha taifa hilo nyuma wakati wa utawala wa Taliban miaka ya 1990 ambapo wanawake walikatazwa kusoma na kufanya kazi.

Wizara ya wanawake yafungwaMnamo Ijumaa, Septemba 17, Taliban ilibadilsha wizara ya masuala ya wanawake na lingine kwa jina “uenezi wa fadhila na kuzuia visa"

Kulikuwa na maandamano ya wanawake nje ya wizara ya masuala ya wanawake kufuatia mabadiliko hayo.

"Hatutaki wizara hii kuondolewa . Kuondolewa kwa wanawake ina maanisha kuwa ni kuondolewa kwa binadamu," ilisoma moja ya mabango.

Maandamano hayo yalidumu kwa dakika 10 na kisha wanawake hao waliingia kwenye magari yao na kuondoka.

Wanajeshi wa Taliban walipindua serikali ya Afghanistan mnamo Jumapili, Agosti 15.

Ilikuwa kipindi ambacho Marekani iliwatorosha raia wa Afghan ambao walikuwa wanatoroka taifa hilo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke