Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Angola yawatimua mapasta zaidi ya 100 kutoka Brazil kwa ufisadi

C42075eec837d55f Serikali ya Angola yawatimua mapasta zaidi ya 100 kutoka Brazil kwa ufisadi

Mon, 17 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- UCKG, linaloongozwa na Edir Macedoni, ni moja ya makanisa makubwa nchini Brazil na matawi 130 katika mataifa tofauti ulimwenguni

- Kanisa hilo linashtumiwa kutekeleza udanganyifu wa kukwepa ushuru na uhalifu nyingine lakini uongozi wa UCKG ulikanusha madai hayo

- Mnamo 2019, inakumbukwa kwamba takriban maskofu 300 raia wa Angola waligura UCKG wakishtumu uongozi mbaya wa Brazil

- Mapasta tisa walifukuzwa nchini humo Alhamisi, Mei 13, huku wengine 100 zaidi wakitazamiwa kuwafuata wiki hii

Serikali ya Angola imeanza kuwatimua mapasta wa Kanisa la Brazil Universal Kingdom of God (UCKG).

UCKG, linaloongozwa na Edir Macedoni, ni moja ya makanisa makubwa nchini Brazil na matawi 130 katika mataifa tofauti ulimwenguni.

Macedoni pia anaaminika kuwa mmoja wa mapasta matajiri zaidi duniani.

Viongozi wa mashtaka nchini Angola walishtaki kanisa hilo kwa kutekeleza udanganyifu ili kukwepa ushuru na uhalifu nyingine lakini uongozi wa UCKG ulikanusha madai hayo.

Mnamo 2019, inakumbukwa kwamba takriban maskofu 300 raia wa Angola waligura UCKG wakishtumu uongozi mbaya wa Brazil.

Mapasta tisa walifukuzwa nchini humo Alhamisi, Mei 13, huku wengine 100 zaidi wakitazamiwa kuwafuata wiki hii.

Ivone Teixeira ambaye ni msemaji wa serikali ya Brazil, alisema waumini 112 wa UCKG wakiwemo mapasta, maskofu, wake zao na wafanyakazi wanatarajiwa kuondoka Angola.

Alisema raia hao wamegawanywa katika makundi ya watu 10 katika ziara ya kurejea Brazil.

Balozi wa Brazil nchini Angola, Rafael Vidal, alikosa hatua ya serikali ya Angola akisema itaharibu uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.

Humu nchini, pasta wa Kanisa la African Divine eneo la Lugari, Kaunti ya Kakamega, ambaye alifumaniwa akifanya ngono na mke wa muumini wake amepigwa ya KSh2,000.

Mhubiri huyo aliyetambuliwa kwa jina Samuel pia alitozwa faini ya ng'ombe na kondoo kama adhabu kutoka kwa baraza la wazee wa jamii ya Kabras.

Samuel alipatikana na hatia ya kuchovya asali ya mke wa Charles Mulongo kwenye kitanda chao cha ndoa katika kijiji cha Mufutu siku ya Ijumaa, Mei 7.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke