Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Seneta mstaafu amtaka Rais Uhuru kuwafuta kazi maboss wa Usalama

Kenyan President Uhuru Kenyatta Seneta mstaafu amtaka Rais Uhuru kuwafuta kazi maboss wa Usalama

Thu, 18 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Aliyekuwa seneta wa Kakamega Boni Khalwale amemtaka Rais Uhuru Kenyatta kuwatimua Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i na katibu wake mkuu Karanja Kibicho kufuatia kisa kilichotokea Kamiti.

Boni Khalwale alitoa kauli yake kufuatia kufutwa kazi kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Wycliffe Ogalo Ogalo Ogalo alikuwa amehusishwa na kudorora kwa usalama katika idara ya urekebishaji tabia na ufisadi.

Aliyekuwa seneta wa Kakamega aliwashutumu Matiang'i na Kibicho kwa kuhusika katika siasa badala ya kuwahudumia Wakenya.

Khalwale, aliyasema haya kufuatia kufutwa kazi kwake Kamishna-Jenerali wa Jeshi la Magereza Wycliffe Ogalo, aliyehusishwa na kudorora kwa usalama katika idara ya urekebishaji tabia na ufisadi.

"Napenda kumpongeza rais kwa hatua aliyoichukua na najua anafahamu kuwa haya ni madhara ya rushwa. Ufisadi uliopo si wa gerezani pekee bali katika idara nzima ya usalama ndio maana tunashuhudia visa kama hivi," alisema Khalwale.

Akizungumza na Citizen TV mnamo Alhamisi, Novemba 18, Khalwale aliwazomea Matiang'i, Kibicho na Mkuu wa Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi (NIS) Meja Jenerali (Rtd) Philip Kameru akisema kuwa wameshindwa kutekeleza majukumu yao.

"Baada ya kuchukua hatua hiyo, nashangaa anafikiria nini kuhusu mkuu wa NIS. Sijui anafikiria nini kuhusu Matiang'i na Kibicho kwa sababu kazi yao ni siasa tu. NIS inapendelea kufuatilia mazungumzo ya simu ya wanasiasa na familia zao na mawasiliano mengine badala ya kushughulikia maswala mengine mazito kama yale ambayo tumeshuhudia hivi punde nchini Uganda," alisema.

Aliwashutumu Matiang'i na Kibicho kwa kuhusika katika siasa badala ya kuwahudumia Wakenya.

"Matiang'i na Kibicho kila wakati wanatumia muda wao kupga domo na siasa tu. Labda rais azingatie kuwaondoa watu hawa kwa sababu usalama wa taifa ni muhimu kuliko sisi sote," akaeleza.

Mnamo Jumatano, Novemba 17 Uhuru Kenyatta amemfuta kazi Kamishna Jenerali wa Magereza, Wycliffe Ogalo, kufuatia kisa cha wafungwa wa ugaidi kutoroka katika gereza la Kamiti.

Taarifa kutoka kwa Msemaji wa Ikulu Kanze Dena ilidokeza kuwa kufutwa kazi kwa Ogalo kulifuatia ukiukaji wa usalama ulioshuhudiwa katika Gereza la Kamiti uliosababisha kutoroka kwa wafungwa watatu.

Hii ilikuwa baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kuhusu kudorora kwa usalama huko Kamiti.

Mkuu huyo wa nchi aliamuru Idara ya Huduma za Urekebishaji kuadhibu hatua za kinidhamu dhidi ya wafanyikazi wote wa Jeshi la Magereza la Kenya waliokuwa kazini ukiukaji wa usalama ulipotokea.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke