Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Seneta Orengo amwaga machungu yake kuhusu siasa za Kenya

3754657ce2f2ebeb Seneta Orengo amwaga machungu yake kuhusu siasa za Kenya

Mon, 10 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Katika ujumbe wake mtandaoni, Orengo ambaye ni mwanchama wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) alisema 'Siasa ya Kenya imejaa uwongo mkubwa uliojaa sauti na ghadhabu ambayo haina faida yoyote'

- Orengo ambaye ni kiongozi wa Wachache katika Seneti alikaa katika kamati ya Pamoja ya Haki na Masuala ya Sheria ambayo ilichukua msimamo tofauti kuhusu BBI

- Mhemko wa Orengo na jinsi alivyobadilika katika siku za karibuni kumeonekana kana kwamba kuna tatizo kubwa ambalo huenda si kuhusu mjadala wa BBI tu

Seneta wa Siaya James Orengo aanayekabiliwa na kipindi kigumu cha siasa kwa mara nyingine ametoa kauli yake kuhusiana na siasa za humu nchini.

Katika ujumbe wake wa facebook, Jumatatu, Mei 10, Orengo ambaye ni mwanchama wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) alisema 'Siasa ya Kenya imejaa uwongo mkubwa uliojaa sauti na ghadhabu ambayo haina faida yoyote'.

Kauli ya wakili maarufu huyo inajiri wakati akionekana kama msaliti katika kambi ya Raila Odinga na ni baada ya kusisitiza kwamba Marekebisho yalipaswa kufanyiwa Mswada wa Mchakato wa Salamu ya Maridhiano (BBI) kabla ya kupitishwa bungeni.

Orengo ambaye ni kiongozi wa Wachache katika Seneti alikaa katika kamati ya Pamoja ya Haki na Masuala ya Sheria ambayo ilichukua msimamo tofauti kuhusu BBI.

"Siwezi kutishwa katika maisha yangu ya Kisiasa kwa sababu nimeona watu wengi wakija na kuondoka. Nimeona watu wengi wenye nguvu." alisema wakati akiwa bungeni.

Kauli yake hiyo ilimfanya kuonekana na kutajwa kichinichini kuwa mwasi katika chama cha ODM.

Mhemko wa Orengo na jinsi alivyobadilika katika siku za karibuni kumeonekana kana kwamba kuna tatizo kubwa ambalo huenda si kuhusu mjadala wa BBI tu.

Baadhi ya wachanganuzi wa masuala ya siasa wanadai kuwa, seneta huyo ni mtu mwenye haraka ya kujiwekea himaya yake mbali na Raila huku safari ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2022 ikiendelea kushika kasi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke