Hii ni baada ya uvumi kusambaa kwenye mtandao wa kijamii Jumapili kuwa mwanasiasa huyo alikamatwa eneo la Hurlingham, Nairobi akipiga sherehe saa za kafyuHata hivyo, Omanga alikanusha madai hayo akisema ni uvumi unaoenezwa na mablogaTaarifa kuhusu kukamatwa kwake kulizua ghadhabu miongoni mwa Wakenya ambao walitaja kama kuhangahishwa kwa wandani wa Naibu Rais William Ruto
Seneta maalum Millicent Omanga amepuzilia mbali madai ya kukamatwa kufuatia uvumi kuenea kuwa alikamatwa kwa kuvunja sheria za kafyu.
Hii ni baada ya penyenye kusambaa kwenye mtandao wa kijamii Jumapili, Julai 25, kuwa mwanasiasa huyo alikamatwa eneo la Hurlingham, Nairobi na maafisa kutoka Kituo cha Polisi cha Kileleshwa.
Katika taarifa kwenye kurasa zake za mtandao wa kijamii siku ya Jumapili, Julai 25, Omanga alikanusha madai hayo akisema ni uvumi unaoenezwa na mabloga.
"Watu wangu mimi niko sawa ka usingizi kananibamba tu...izo zingine ni story," aliandika Omanga.
Read also
Mheshimiwa Gachagua Apigwa na Kibaridi Sakafuni Seli, Kushtakiwa Jumatatu
Gachagua alikamatwa byumbani kwake Nyeri na makachero kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai.
Gachagua anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Gigiri na anatazamiwa kufikishwa kortini hii leo Jumatatu, Julai 26.
Wandani wa Ruto wazuiwa kumuona GachaguaWandani wa Naibu Rais William Ruto ambao walifika katika kituo hicho cha Gigiri hawakuruhusiwa kumuona mheshimiwa.
Mwanablogu wa mrengo wa DP Ruto Dennis Itumbi alisema OCPD wa kituo hicho aliwaarifu kuwa mkuu wa DCI George Kinoti alikuwa na amri asiruhusu Gachagua kuongea na yeyote.
"OCPD wa Gigiri na DCIO walituarifu kuwa mkuu wa DCI George Kinoti amepewa amri kuwa marafiki na wabunge wasipate nafasi ya kumuona au kuzungumza na Rigathi," alisema Itumbi.
Mbunge huyo anakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na utapeli wa pesa.
Read also
DPP Haji Akana Madai kwamba Aliamuru Kukamatwa kwa Jaji Muchelule na Chitembwe
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke