Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Seneta Kang'ata asema Raila ni mvivu, ameshindwa kutafuta kura Mlima Kenya

F3f4545cdbe8ef5f Seneta Kang'ata asema Raila ni mvivu, ameshindwa kutafuta kura Mlima Kenya

Thu, 3 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Seneta Kang'ata alipuzilia mbali madai kuwa Raila Odinga amekataliwa katika eneo la Mlima Kenya kwa sababu ya ukabila

- Alimuomba kiongozi wa ODM kutembelea eneo hilo na kujishirikisha na wakazi

- Raila bado hajatangaza wazi endapo atawania urais lakini kaka yake Oburu Odinga alidokezea awali kwamba atakuwepo kwenye kivumbi cha 2022

Seneta wa Murang'a Irungu Kang'ata amemchamba waziri mkuu wa zamani Raila Odinga akimuelezea kama mwanasiasa 'mvivu'.

Akizungumza na Citizen TV Jumayano, Juni 2, Kang'ata alipuzilia mbali madai kuwa kiongozi huyo wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) amekataliwa katika eneo la Mlima Kenya kwa sababu ya ukabila.

"Dhana kuwa watu wa Mlima Kenya hawampendi Raila Odinga kwa sababu ya ukabila si kweli kabisaa.Ukiangalia kipindi kati ya 2008 na 2009, nani ndio hakuwa na umaarufu eneo letu? Pengine niseme William Ruto," alisema Kang'ata.

"Lakini mbona Ruto amekuwa maarufu eneo letu? Ni kutokana na uvivu kisiasa. Raila amekuwa akikaa Nairobi akisubiri kupendekezwa na wanasiasa wakuu kutoka Kikuyu jijini ," Kang'ata alidai.

Kiranja huyo wa zamani wa wengi Seneti alihoji kuwa Raila anatumaina kutumia handisheki kati yake na Rais Uhuru Kenyatta kujishirikisha na watu wa Mlima Kenya.

Kang'ata ambaye alihamia kambi ya Ruto baada ya kuadhibiwa na Chama cha Jubilee, alisema Naibu Rais ameweza kujipatia umaarufu eneo hilo kwa sababu ya kuzungumza na wakazi moja kwa moja.

"Endapo Raila anataka kuungwa mkono katika eneo letu ni rahisi, wacha akuje kwetu, akuje kwa harusi zetu, matanga na kuzungumza na watu moja kwa moja.Usikae tu Nairobi ukingoja kupendekezwa," alisema.

Raila bado hajatangaza wazi endapo atawania urais lakini kaka yake Oburu Odinga alidokezea awali kwamba atakuwepo kwenye kivumbi cha 2022.

Akizungumza akiwa katika kituo cha polisi cha Kowet Kaunti ya Siaya, Oburu alisema kilichokuwa kikimfanya kiongozi huyo wa ODM kupoteza chaguzi ni kwa sababu ya hakuwa akipata uungwaji mkono na 'mifumo' almaarufu system lakini sasa kupitia kwa Uhuru, huenda akapata.

"Kwa nini hatuingia Ikulu hata baada ya kushinda, ni kwa sababu kulikuwao na kitu tulichokuwa tukikosa. Ni mfumo. Mfumo ni muhimu na sasa tuna Uhuru Kenyatta ambaye ameshikilia mfumo," alisema Oburu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke